Nutrition Aug 2, 2024

Vyakula vitano vinavyosaidia kupunguza kiungulia

Medikea Clinic

Medikea Clinic

Medical Expert

13617
Vyakula vitano vinavyosaidia kupunguza kiungulia

Kiungulia ni nini na kinasababishwa na nini? Kiungulia ni maumivu ya moto kwenye kifua, nyuma ya mfupa wa kifua. Maumivu haya hutokea baada ya kula, wakati wa kulala au wakati mtu ameinama.

Kiungulia hutokea wakati asidi ya tumbo inaporudi kwenye umio, mrija unaosafirisha chakula kutoka mdomoni hadi tumboni

KIUNGULIA KINAWEZA KUCHOCHEWA NA VITU KAMA VILE:

  • Vyakula vya mafuta au vya kukaanga.

  • Vinywaji vya kaboni, pombe, kahawa na vinywaji na vinywaji vya kafeini.

  • Bidhaa za machungwa.

  • Bidhaa za nyanya.

  • Chocolate

  • Milo mikubwa.

Ili kupunguza kiungulia inabidi kula vyakula vyenye asidi kidogo katika milo ya kila siku.

VYAKULA VITANO VINAVYOSAIDIA KUPUNGUZA KIUNGULIA

  • Vyakula vya alkali (Alkaline food): Vyakula hivi vina kiwango cha chini sana cha asidi hivyo husaidia kupunguza tatizo la kiungulia. Vyakula vya alkali huhusisha matunda kama vile ndizi na matikitiki, fenesi na karanga.

  • Tangawizi: Tangawizi ni mojawapo ya chakula cha asili kinachosaidia kupunguza tatizo la kiungulia. Tangawizi zina vitamin C na B, madini ya chuma, madini ya zink magnesium, calcium na phosphorus ambavyo pia hutumika kutibu tatizo la gesi tumboni na kiungulia.

  • Nyama zisizo na mafuta: Nyama kama vile kuku, bata mzinga na samaki hazina mafuta mengi hivyo zinaweza kutumika kupunguza hatari ya kiungulia kama zikichomwa au kuokwa. Hivyo ni vyema kuepuka kuzikaanga kwani vyakula vya kukaanga vina mafuta mengi na ni moja ya sababu kuu ya kiungulia.

  • Vyakula vya nafaka nzima: Vyakula vya nafaka nzima kama vile oatmeal, mkate na wali wa kahawia ni njia nzuri za kupambana na kiungulia kwani zinasaidia kunyonya asidi iliyojaa ndani ya tumbo, na nafaka hizi zimejaa vitamini na madini.

  • Maziwa mtindi: Maziwa ya mtindi ambayo hayana mafuta mengi husaidia kuzuia kiungulia na pia yana bakteria wazuri ambao huboresha usagaji wa chakula.

MUHIMU:

Ni vyema ukapata ushauri wa daktari kwanza kabla ya kuendelea na tiba yoyote ya mitishamba, kwa sababu vyakula vingine vinaweza kuwa na madhara kwako na mwingiliano wa madawa. Unaweza ku chat na daktari kupitia Medikea App.

Related Articles

No related articles found.

More Health Insights

Vyakula vitano vinavyosaidia kupunguza kiungulia
Nutrition

Vyakula vitano vinavyosaidia kupunguza kiungulia

Kiungulia ni hali inayotokea kwa watu wengi. Soma makala hii kujifunza zaidi.

13617
Aug 2, 2024
Read More
Tiba ya bawasiri (Hemorrhoids)
Men

Tiba ya bawasiri (Hemorrhoids)

Bawasiri inasababishwa na nini, dalili zake, na jinsi ya kuzitibu

13245
Aug 30, 2023
Read More
Kupungua Kwa Kumbukumbu: Sababu Na Jinsi Ya Kukabiliana Nayo
Chronic diseases

Kupungua Kwa Kumbukumbu: Sababu Na Jinsi Ya Kukabiliana Nayo

Una wasiwasi kuhusu kupungua kwa kumbukumbu kwako au kwa mpendwa? Pata ushauri wa kitaalam kupitia application ya afya y ...

1370
Feb 25, 2025
Read More