Women Aug 12, 2024

Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Medikea Doctor

Medikea Doctor

Medical Expert

4710
Huu Ndio Utaratibu wa Kufanya Mazoezi Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Kuwahi kutembea na kurudia shughuli za kawaida na za kabla ya ujauzito na kujifungua pamoja na mazoezi mara tu daktari anapoona ni salama inasaidia kuimarisha afya ya mama na kupunguza magonjwa yatokanayo na kukaa muda mrefu.

Hata hivyo wanawake wenye matatizo yafuatayo wanashauriwa kuchelewa kidogo kurudia mazoezi na shughuli za awali kabla ya ujauzito na wapate idhini ya daktari kabla ya kuanza kutembea au kufanya mazoezi

• Wenye magonjwa mengine (upungufu wa damu, magonjwa ya moyo na njia ya hewa, matatizo ya damu kuganda kwenye mishipa) • Wana maumivu na bado wanahitaji dawa za kutuliza maumivu • Madhara wakati wa na baada ya upasuaji (kichefuchefu na kutapika, kidonda kutopona vizuri, ganzi, mkojo kutoka wenyewe)

Sasa kwa wale ambao hawana matatizo na wale ambao wamepata idhini kutoka kwa daktari utaratibu wa kufanya mazoezi uko hivi :

▪️Wiki ya 1 hadi wiki ya 2 baada ya kuruhusiwa

  • Tembea angalau dakika 10 kwa siku mara nyingi kadri uwezavyo na unaweza kuongeza muda kadri unavyoweza

  • Panda ngazi nyumbani au hospital ukiwa na msaidizi

  • Usinyanyue kitu kingine chochote chenye uzito zaidi ya uzito wa mtoto

▪️Baada ya wiki 3 na kuendelea

Fanya mazoezi ya kuimarisha nyonga na tumbo

Angalia video za mazoezi yafuatayo YouTube (Pelvic tilting and abdominal curl,Lower back lift, Oblique curls, Lateral tilts, Kegel pelvic floor muscle). Fanya mazoezi katika kila kundi kuanzia mara 10 hadi 12 kwa kuanza taratibu na kuongeza kadri uwezavyo.

▪️Baada ya wiki 6 na kuendelea

-Wanawake ambao hapo awali walikuwa wanafanya mazoezi kwenye gym na vilabu vya mazoezi taratibu na kwa uangalifu wanaweza kurudia mazoezi yao kwa kuanza na settings za chini kwenye mashine za mazoezi

-Baada ya wiki sita wanawake wote wanaweza kufanya mazoezi ya kiwango cha kati (moderate intensity physical activity) kama inavyopendekezwa kwa watu wengine ambayo ni kufanya mazoezi hayo kwa muda wa dakika 150 hadi 300 kwa wiki)

Kwa msaada wa karibu wa mtaalamu wa mazoezi (Physiotherapist) pakua app ya Medikea ku chat au wasiliana na Medikea Clinic kupitia 0763100093 ili kupata mazoezi tiba clinic au nyumbani!

Related Articles

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga
Women

Uti ni nini? Dalili zake na jinsi ya kujikinga

UTI inasababishwa na nini, dalili zake na jinsi ya kujinga

48182
Nov 6, 2024
Read More
Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha
Women

Ijue siri kubwa ya kuzalisha maziwa ya kutosha

Soma kujua jinsi ya kuzalisha maziwa ya kutosha kwa mama anaenyonyesha!

2206
Aug 28, 2024
Read More
“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili
Women

“Tayari Nina Watoto Lakini Sipati Tena Mimba” - Ugumba wa aina ya pili

Fahamu sababu zinazosababisha ugumba kwa wenza ambao wameshapata Mtoto awali

1001
May 15, 2024
Read More

More Health Insights

Dalili za Mimba Wiki ya Kwanza
Pregnancy

Dalili za Mimba Wiki ya Kwanza

Ujauzito ni mchakato wa kibaiologia ambao unahusisha mabadiliko makubwa katika mwili wa mwanamke. Katika wiki ya kwanza, ...

15345
Feb 25, 2025
Read More
Wegovy (Ozempic): Dawa mpya za kupunguza uzito, inafanya kazi? Je ni salama?
Wellness

Wegovy (Ozempic): Dawa mpya za kupunguza uzito, inafanya kazi? Je ni salama?

Ozempic, wegovy, maunjaro na dawa nyingine za kupunguza uzito

1675
Aug 9, 2024
Read More
Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito
Pregnancy

Jinsi ya Kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito

Jifunze njia za kupunguza Kichefuchefu na Kutapika wakati wa Ujauzito⁣

9227
Aug 28, 2024
Read More